Ijumaa , 15th Dec , 2017

Kocha wa Manchester City Pep Guardiola ameendelea kuweka rekodi katika ligi kuu ya soka nchini England (EPL) baada ya kushinda tuzo ya kocha bora wa mwezi Novemba.

Kwa kushinda tuzo hiyo leo, Guardiola sasa ameweka rekodi ya kuwa kocha wa kwanza kuchukua tuzo hiyo mara tatu mfululizo. Mhispania huyo ameshinda katika miezi ya Septemba, Oktoba na Novemba ambayo ameshinda leo.

Pep amechukua tuzo hiyo leo akiwashinda waliokuwa wapinzani wake kwenye kuwania tuzo hiyo Antonio Conte, Sean Dyche, Jurgen Klopp, Jose Mourinho na Arsene Wenger.

Jumatano wiki hii Pep aliweka rekodi ya kuwa kocha wa kwanza kushinda michezo 15 mfululuizo kwenye EPL na kuzikaribia rekodi zake mwenyewe ambazo amewahi kuziweka kwenye ligi za La Liga (16) na Bundesliga (19).