
Rais mpya wa TBF Michael Kadebe wakati akijinadi kuomba kura
Kwenye nafasi ya makamu wa Rais Rwehabura Barongo ambaye ni MVP wa kwanza wa michuano ya Sprite Bball Kings inayoandaliwa na East Africa TV na East Africa Radio, ameshinda nafasi hiyo baada ya kupigiwa kura 44, akiwashinda Mboka Mwambusi aliyepata kura 9 na Alphonce Kusekwa kura 7.
Rwehabura Barongo
Mwenze Fiston ameshinda nafasi ya katibu mkuu wa TBF kwa kura 47, akimshinda Michael Mwita 13 na nafasi ya katibu msaidizi ameshinda Benson Nyasebwa kwa kura 50 dhidi Daniel Kapomaaliyepata kura 10.
Wajumbe 60 ndio waliopiga kura kwenye uchaguzi huo, na safu mpya ya uongozi italiongoza shirikisho hilo kwa miaka 4 ijayo.