Jumatatu , 30th Mei , 2022

Jayson Tatum ametangazwa kuwa mchezaji bora (MVP) wa fainali ya Ligi ya mpira wa kikapu nchini Marekani NBA ukanda wa mashariki baada ya kuiongoza Boston Celtics kufuzu kucheza fainali ya NBA msimu huu.

Tatum ameshinda tuzo ya MVP ya Larry Bird kanda ya Mashariki

Tatum amefunga alama 26, pasi za kufunga 6 na rebound 10. Kwenye mchezo wa 7 wa fainali ukanda wa mashariki dhidi ya Miami Heat ambao wameshinda kwa alama 100 kwa 96.

Kwenye mfululizo wa michezo 7 ya fainali Tatam mwenye umri wa miaka 24 amekuwa na wastani wa kufunga alama 24.8, rebound 8 na pasi za kufunga (assists) 5.5 kwa mchezo. Tuzu ni mpya na Tatumamekuwa mchezaji wa kwanza kushinda na inabeba jina la mchezaji wa zamani wa Boston Celtics Larry Bird