Lukaku ameomba msamaha baada ya kuonesha hisia zake chanya juu ya mbinu za kocha wake zinazombelekea Mbelgiji huyo kukosa nafasi ya kuanza kwenye kikosi cha kwanza mara kwa mara ambapo Kai Havertz amekuwa akitumika mara nyingi kama namba tisa.
Kufuatia mazungumzo ya Lukaku na kocha wake Tuchel , mchezaji atazamiwa kulipa faini ya Euro Laki sita sawa sawa na Billion 1.5 za kitanzania ikiwa kama adhabu ya kuvunja sheria za matumizi ya viombo vya habari za klabu ya Chelsea pamoja na kukomesha tabia hiyo ya kumzungumzia kocha wake vibaya.
Lukaku aliachwa nje ya kikosi cha Chelsea walipocheza dhidi ya Liverpool kwenye mchezo uliomalizika kwa sare ya 2-2.
