Jumatano , 11th Jan , 2023

Waziri wa afya wa Uganda Jane Ruth Aceng ametangaza rasmi kumalizika kwa mlipuko wa Ebola ulioanza miezi mitatu iliyopita na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 50

Kisa cha kwanza cha mgonjwa wa Ebola kilithibitishwa katika wilaya ya Mubende mwezi Septemba mwaka jana
Shirika la afya duniani WHO limethibitisha taarifa hiyo ya kumalizika kwa Ebola Uganda

Kwa mujibu wa WHO, taifa hutangazwa kumaliza Ebola iwapo hakujatokea kisa chochote katika kipindi cha siku 42 mtawalia

Aidha WHO imesema Uganda ilisajili visa 142 vya Ebola, vifo 55, wagonjwa 87 wakiripotiwa kupona.