Mtoto amkatakata baba yake kwa shoka
Jeshi la Polisi mkoa wa Tabora linamshikilia kijana Michael Jacobo (25) mkazi wa Kijiji cha Upungu wilaya ya Nzega kwa tuhuma kumuua baba yake mzazi Jacobo Lubela, baada ya kumvizia majira ya jioni akiwa nje ya nyumba na kumkata shoka kichwani, shingoni na mikono yote miwili.

