Medvedev kupambana na Nadal Mexico Open
Michuano ya wazi ya Mexico (Mexican Open) imeingia hatua ya nusu fainali ambapo nyota kutoka nchini Urusi Daniil Medvedev atacheza dhidi ya Mhispania Rafael Nadal kwenye nusu fainali ya kwanza na mchezo huo ukikumbushia mchezo wa fainali wa michuano ya wazi ya Australian 2022.

