Simiyu kuiingiza Tanzania 10 bora Duniani
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu David Kafulila amesema mkoa huo utaiingiza Tanzania miongoni mwa Mataifa 10 yatakayozalisha pamba kwa wingi duniani mwaka ujao na kuyazidi mataifa kama Burkina Faso na Benin ambayo yanafanya vizuri katika uzalishaji wa pamba barani Afrika.