Simba SC wametua salama Niger, tayari kwa mchezo
Kikosi cha Simba SC kimefika salama nchini Niger leo jioni tayari kwa mchezo wa kombe la shirikisho barani Afrika dhidi ya wenyeji wao US Gendarmerie. Timu hizi mbili zitashuka dimbani kesho kuwania alama 3 katika muendelezo wa michezo ya hatua ya makundi.

