Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Lema atumia dakika 44 kumjibu Zitto

Tuesday , 16th Oct , 2018

Waziri Kivuli wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Godbless Lema ametumia dakika 44 kujibu lililokuwa hitaji la Mbunge wa Kigoma mjini, Zitto Kabwe juu ya kutoa tamko kuhusu tukio la kupotea kwa mfanyabiashara maarufu
nchini Mohamed Dewji.

Godbless Lema

Hivi karibuni Zitto alikuwa akimshinikiza Mbunge huyo wa Arusha mjini kuzungumza juu ya taarifa ya matukio ya kupotea kwa watu siku chache kufuatia kupotea kwa Mo Dewji ikiwa ni baada ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Kangi Lugola kusema kuwa katika kwa kipindi cha Miaka 3 zaidi ya watu 75 walitajwa kupotea.

Katika mkutano na wanahabari leo jijini Dar es salaam, Godbless Lema amesema kuwa tukio la kupotea kwa mfanyabiashara huyo linaathiri taswira ya Tanzania hasa kwenye masuala ya uwekezaji.

Watu wengi duniani wameona tukio la kidnaped (utekaji), leo hii habari zinaenda kwa matajiri duniani, hawa ndio wanahamasisha uwekezaji, mmeona kwenye vyombo vikubwa vya habari duniani. Matokeo yake kwenye uchumi ni kubwa mno, kama tungekuwa kwenye stock market(soko la hisa) mngeona shilingi inashuka. Watu wenye mitaji wataondoa mitaji yao kwa ajili ya kukwepa usalama wataenda kwenye nchi jirani”, amesema Lema.

Kupitia mtandao wa Twitter, Zitto Kabwe aliandika "ndugu @godbless_lema kwenye utamaduni wa Jumuiya ya Madola, Waziri mwenye dhamana akitoa kauli, lazima Waziri Kivuli wa sekta hiyo atoe kauli pia ama kuunga mkono au kupingana na ya Waziri mwenye dhamana, tunasubiri kauli yako. Nchi inasubiri. Kukaa kimya nikukubaliana na Kangi."

Alhamis ya wiki iliyopita kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii nchini kulianza kusambaa taarifa juu ya kupotea kwa Mfanyabiashara maarufu nchini Mohamed Dewji ambaye inasemekana amechukuliwa na watu wasiojulikana.

Jeshi la Polisi hii leo limewaachia kwa dhamana watu 19 kati ya 26 ambao walikamatwa kwa mahojiano, akiwemo Afisa Habari wa klabu ya Simba, Haji Manara ikiwa ni sehemu ya upelelezi wa tukio la kutekwa kwa mfanyabiashara huyo. Familia ya Mohammed Dewji imetangaza kutoa donge nono la shilingi bilioni 1 kwa atakayesaidia kutoa taarifa za ukweli za kupatikana kwake.

HABARI ZAIDI

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu