Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mbunge atolewa kwa dirishani na Polisi

Monday , 22nd Apr , 2019

Mbunge wa Kyadondo Mashariki Robert Kyagulanyi  'Bobi Wine' amekamatwa baada ya yeye na wafuasi wake kugombana na maafisa wa polisi kufuatia hatua ya mamlaka kufutilia mbali tamasha lake la muziki la siku kuu ya pasaka.

Mbunge wa Kyadondo Mashariki Robert Kyagulanyi  'Bobi Wine'.

Kulingana na gazeti la Daily Monitor nchini Uganda Mbunge wa Makindye Magharibi Allan Ssewanyana alizirai na ikalazimika wafuasi wake kumbeba hadi katika gari moja ambalo lilikuwa likimsubiri.

Hali ya wasiwasi ilitanda baada ya maafisa wa polisi kuuzuia msafara uliokuwa ukiongozwa na mbunge huyo katika tamasha lake la One Love huko Busabala.

Wawili hao walikamatwa mapema siku ya Jumatatu na kuzuiliwa katika gari moja la maafisa wa polisi kabla gari hilo kuondoka nao.

Kukamatwa kwa Bobi Wine kunajiri baada ya rais Yoweri Museveni kusema kuwa hatokubali matamasha ya muziki uliojaa siasa na kuonya kwamba katika siku za usoni hakuna mtu atakayefidiwa kwa matamasha ambayo yamefutiliwa mbali kutokana na siasa.

Bobi Wine alikamatwa na kuingizwa katika gari la polisi na kupelekwa eneo lisilojulikana.

Awali polisi walitumia nguvu kulifungua gari ambalo mbunge huyo kabla ya kuvunja vioo vyake na kumtoa nje.

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea