Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Uganda kuanza kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa ng'ombe

Thursday , 18th Jul , 2019

Serikali nchini Uganda imedhamiria mpango wa kuwasajili wakulima na ng'ombe wao kwa ajili ya kurahisisha utambuzi na kuwawezesha fursa za soko la Kimataifa.

Ng'ombe

Hayo yameelezwa na Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Vincent Ssempijja alipokuwa akizindua maonesho ya wakulima katika viwanja vya Nile mjini Jinja, ambapo amesema soko la Kimataifa linataka nchi zinazozalisha mazao hayo kusajili.

"Wanahitaji kujua bidhaa wanazonunua zinatoka wapi, wamekuwa wakikataa kulipa na kuzuia bidhaa zilizosafirshwa kutoka Uganda pindi wanakuta boksi moja lina shida", amesema Waziri Ssempijja.

"Wakulima watasajiliwa na bidhaa wanazozalisha zitapewa utambuzi wa 'barcodes', ili kama wakigundua box lina kasoro, wafuatilie chanzo na kurekebisha. Hatuwezi kuingia katika soko la aina hiyo hadi hapo tutakapowasajili".

Pia kuhusiana na suala la usajili wa ng'ombe, Waziri huyo wa Kilimo amesema, "kwa wafugaji wa ng'ombe watasajiliwa wenyewe na ng'ombe wao pia watasajiliwa na kupewa vyeti vya kuzaliwa kwa sababu walaji wanahitaji nyama ya ng'ombe yenye umri kati ya miezi 15 hadi 24. Kwahiyo tunakwenda kuuza kutokana na umri wao".

Kilimo ni moja ya sekta muhimu katika uchumi wa nchi ya Uganda kwa masuala ya ajira na chakula, huku kikichangia asilimia 25 ya ukuaji wa pato la ndani la taifa (GDP).

HABARI ZAIDI

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu