Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wananchi wakimbia hospitali kisa waganga wa jadi

Friday , 15th Feb , 2019

Changamoto ya upatikanaji wa huduma za Afya katika kijiji cha Nyang’holongo Kata ya Nundu Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale Mkoani Geita imekuwa kubwa, hali inayopelekea wananchi kukimbilia kwa waganga wa jadi kupata huduma hizo.

Baadhi ya vifaa vya waganga wa jadi

Imeelezwa kuwa sababu za baadhi ya wananchi kufuata huduma za matibabu kwa waganga wa jadi ni huduma za afya kuwa umbali mrefu kwani wanalazimika kutembea umbali wa kilomita 10 kwenda katika Zahanati ya kata jirani ya Bukwimba ama wanasafiri kwenda makao makuu ya Wilaya kwenye kituo cha afya Kharumwa takribani kilomita 25.

Marko Mwiyabule ni Mwenyekiti mwanzilishi wa kijiji hicho tangu mwaka 1974 na kustaafu mwaka 2004, ambapo  anasema wananchi wamekuwa wana mwamko hali iliyopelekea kuchangia  Sh. elfu sitini kwa lengo la kujenga zahanati ambapo afisa Mtendaji wa Nyang’holongo Masumbuko Robert amesema walifikisha milioni 22 ambazo walinyanyua boma.

Kutokana na changamoto hizo zinazowakabili wananchi, Mgodi wa Dhahabu wa Acacia Bulyanhulu kutoka Mkoani Shinyanga umeguswa na kutoa msaada wa vifaa vya ujenzi vyenye thamani ya zaidi ya Milioni 67.

Akipokea vifaa hivyo Mkuu wa wilaya ya Nyang’hwale, Hamimu Gwiyama amesema kiongozi kutoka ngazi ya wilaya kwa mara ya mwisho alifika kijijini hapo mwaka 2005 yapata miaka 14 sasa.

Aidha uongozi wa kijiji umesema kuna wakazi wapatao 2598 na kwamba waliochangia fedha kama nguvu za wananchi ni wakazi 502 hivyo wamejielekeza kuleta msukumo zaidi ya ili watu wote washiriki kikamilifu kwenye miradi ya maendeleo.
 

HABARI ZAIDI

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu