Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

WB yatoa mkopo kwa masharti kwa watoto wa kike

Sunday , 18th Nov , 2018

Baada ya kuzungumza na Serikali, makamu wa Rais wa Benki ya Dunia (WB) Kanda ya Afrika, Dkt. Hafez Ghanem amesema kuna masharti wamekubaliana kabla Tanzania haijapewa mkopo wa Dola 300 milioni za Marekani kwa ajili ya kuboresha elimu nchini.

Makamu wa Rais wa WB Kanda ya Afrika, Dkt. Hafez Ghanem, akiwa na Rais Dkt. Magufuli, Ikulu jijini Dar es salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari, Dkt.  Ghanem amesema benki hiyo inatoa fedha kwa ajili ya wasichana wote bila kujali hali zao, hivyo kuwatenganisha kwa kigezo cha ujauzito au kingine chochote ni kwenda kinyume na mkakati wa elimu jumuishi.

Wataalamu wetu watashirikiana na serikali kuona ilivyojiandaa kutoa elimu kwa wasichana wote, tutakapojiridhisha bodi ya wakurugenzi itaidhinisha mkopo husika na kuchelewa kwake kutategemea lini serikali itatekeleza masharti tuliyokubaliana", amesema Dkt. Ghanem.

Mkopo huo ilikuwa ujadiliwe na kuidhinishwa Oktoba 30, lakini kutokana na msimamo wa serikali kutotoa fursa ya kuendelea na masomo wasichana wanaopata mimba, bodi ya benki hiyo ilisitisha kuujadili. Kwa utaratibu wa benki hiyo, kabla mradi wowote haujaidhinishiwa fedha zinazohitajika, huujadili kwanza.

Novemba 16, baada ya mazungumzo na makamu wa Rais wa Benki ya Dunia (WB), Rais Magufuli alisema kuwa Benki hiyo imeridhia kuipatia Tanzania Dola za Marekani milioni 300 sawa na shilingi bilioni 680.5  kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa kuongeza ubora wa elimu ya sekondari, ambapo zitatumika katika ujenzi wa madarasa, mabweni, maabara, nyumba za walimu na vifaa vya kufundishia.

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea