
Akiwa KIKAANGONI East Africa Television, Ebitoke amesema kuwa licha ya kwamba hivi sasa hayuko tena kwenye mahusiano na Ben Pol, lakini yeye ndiye alikuwa mwanaume wake wa kwanza na ndiye aliyempa zawadi ya usichana wake aliyomuahidi.
“Kama ulimuahidi mtu zawadi lazima umpe, nimeshampa Ben Pol zawadi yake”, amesema Ebitoke.
Ebitoke amesema kwamba wawili hao kwa sasa hawako pamoja lakini wanaendelea kusaidiana kwenye kazi, na sio kimapenzi tena.
Ikumbukwe kwamba baada ya Ebitoke kukiri kuwa na hisia za kimapenzi kwa Ben Pol aliweka wazi kuwa yeye bado ni msichana na usichana wake alitunza kwa ajili yake, hivyo kama angekuwa naye yuko tayari kumpa.
Kuwa supa na Instagram ya bure toka Vodacom kwa kununua kifurushi cha kuanzia buku tu.