Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Umri wangu sio tatizo - Mwasiti

Wednesday , 15th Aug , 2018

Msanii wa Bongo Fleva Mwasiti Almasi, amefunguka na kudai umri wake hauwezi kuwa tatizo la yeye kutokuendelea kujihusisha na masuala ya muziki kwa kuwa ana imani bado ana uwezo mkubwa wa kuitendea haki sanaa.

Mwasiti

Mwasiti ametoa kauli hiyo kwenye kipindi cha Planet Bongo kinachorushwa na East Africa Radio leo Agosti 15, muda mchache alipomaliza kutambulisha wimbo wake mpya wa 'Mapene' ulioandikwa na Marioo kwa kushirikiana na yeye mwenyewe huku ukitayarishwa na Kimambo.

"Sijawahi kukata tamaa na muziki, bado nina uwezo wa kuufanya. Toka nimeanza muziki naweza kusema nimeweza kutimiza zaidi ya asilimia 60 ya malengo yangu. Umri sio tatizo katika kufanya kazi maana hata ukimuangalia Joseph Haule 'Prof. Jay' ni Mbunge lakini 'still' anaendelea kufanya muziki", amesema Mwasiti.

Pamoja na hayo, Mwasiti ameendelea kwa kusema "hata nje ya nchi kuna wasanii wenye umri mkubwa lakini huwasikii wameacha kufanya kazi, licha ya kuwa kuna umri ukifika huwezi kuendelea kuonekana juu ya majukwaa kufanya show".

Kauli hizo za Mwasiti zimekuja baada ya wadau wengi kuamini vichwani mwao, kuwa wasanii wa zamani hawana uwezo wa kuendelea kimuziki katika nyakati za sasa, kutokana na kuwepo wimbi kubwa la wasanii chipukizi na kubadilika soko la kibiashara.
 

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea