Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Afikia mshindo mara 50 kwa siku

Thursday , 17th Jan , 2019

Msichana Amanda Gryce, mkazi wa Florida nchini Marekani, anasumbuliwa na ugonjwa ambao sio wa kawaida, unaomfanya afikie mshindo takriban mara 50 kwa siku, bila ya kufanya tendo la ndoa na mtu yeyote.

Msichana huyo mwenye miaka 22, anasema alianza kugundua ana tatizo hilo akiwa na miaka 6, na amekuwa akikabiliana nalo bila kujua hatma yake ni nini, na amekuwa akikutwa na hali hiyo muda wowote na mahali popote bila kufanya tendo la ndoa.

“Ilitakiwa iwe ni kitu kizuri kama ambavyo inatakiwa, imekuwa maumivu kwangu, kwa sababu inatokea sana,  inaweza ikatokea hata mara 50 kwa siku au mara tano mpaka kumi kwa saa moja, inatokea nikiwa na rafiki zangu, au nikiwa sehemu tu na watu wengine, nikipanda gari ndio inazidi kutokana na mtikisiko wake, ni aibu sana”, amesema Amanda.

Tatizo hilo ambalo mwenyewe anadai limekuwa likimtesa maisha yake yote na kumfanya asifurahie maisha ya kimapenzi, kilimfanya awahi kuwaza kujiua, lakini mpenzi wake Stuart Triplett, amekuwa akimpa ushirikiano sana wa kutafuta tiba na kumfanya awe na tumaini.

Kutokana na hali hiyo, Amanda ameshakutana na baadhi ya madaktari kujaribu kupata tiba, lakini mpaka sasa hajapata ufumbuzi kutokana na ugonjwa huo kutokuwa na tiba ya moja kwa moja, hivyo kumpa njia mbadala za kukabliana nao, ikiwemo kufanya mazoezi.

Tatizo hilo kitaalamu linajulikana kama 'Persistent Genital Arousal Disorder'ambalo hutokea mara chache sana kwa binadamu. Mpaka sasa haujajulikana tiba sahihi ya kuweza kumaliza tatizo hilo, lakini madaktari wa masuala hayo wameshauri iwapo mtu atagundulika kuwa na tatizo hilo, atatakiwa kuhudhuruia tiba ya mwili 'Physiotherapy'.

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea