Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Madhara ya kujichubua kwa watumiaji

Tuesday , 25th Sep , 2018

Watu wengi hususani wanawake hupenda kuonekana wakiwa warembo, huku miongoni mwao wakiwa na dhana potofu ya kwamba ili uwe mrembo ni lazima ung'arishe rangi ya ngozi yako(Ujichubue).wapo wale wenye usemi ya baadhi ya wanaume kupenda wanawake weupe tamaa ambazo hupelekea-

Pichani ni ngozi iliyoathirika na vipodozi.

shinikizo la wanawake hao kutafuta vipodozi vya kupunguza weusi.

VIPODOZI VINAVYOTUMIKA KUJICHUBUA...

Vipodozi hivi huja katika aina tofauti,Wapo wanaotumia mafuta au dawa ya kung'arisha ngozi zao (lotion) au kumeza tembe. Au kama linavyojulikana kwa jina la Mkorogo. Suala hili linanipa motisha ya kulizamia kwa kina kujua athari za matumizi ya madawa ya kubadilisha ngozi ama kujichubua. (skin bleaching)

 KEMIKALI SUMU NDANI VIPODOZI...

Katika bidhaa zinazotumika kujichubua, kuna kemikali za aina mbili. Ambayo ni ‘Hydroquinone’ na ‘Mercury’
Hydroquinone kemikali hii ni sumu kali, ambayo hutumika kwa ajili ya kuchapisha picha na kutengeneza bidhaa za mpira. pia kama kisaidizi katika kutengeneza rangi za nywele. Mercury nayo ni kemikali ya sumu inayoweza kuuzwa katika maduka ya madawa.

 MADHARA YA KUJICHUBUA...

Katika kujichubua yapo madhara mbalimbali yanayowakumba watumiaji wa vipodozi hivyo;

Dkt. Elizabeth Kilili, ni mtaalamu na Mkurugenzi Mtendaji wa Grace Product Limited ambaye ameainisha madhara yatokanayo na matumizi ya vipodozi hivyo ambayo ni pamoja na kupata kansa ya ngozi, kuzeeka mapema,kupata watoto wenye kasoro, mishipa ya fahamu,figo, kupungua kwa uzito na kupelekea athari za kuvunjika mifupa.Madhara haya huoneka mara moja na kadri mtu anavyozidi kutumia mkorogo kung'arisha ngozi yake.

Pia Dkt Kilili amesema, _“__upande wa mama mjamzito vipodozi venye viambata sumu vina muathiri mtoto kwenye mfumo wake wa chakula kupitia kitovu cha mama, kwa sumu inavyopita huelekea kwenye damu ambayo mtoto anapokuwa anazaliwa hutoka na kasoro tofauti ambazo huleta madhara katika ukuaji wake.”_

USHAURI WA KUZINGATIA...

Dkt Kilili anaendelea kwa kutoa ushauri wa kuepukana na madhara ya kujichubua huku akishauri matumizi ya bidhaa za asili zisizokuwa na madhara, ikiwemo kutumia vipodozi vilivyopitishwa na Mamalaka ya Chakula na Dawa (TFDA) pamoja na kupata ushauri kwa wataalamu juu ya afya na magonjwa ya vipodozi ikiwemo kujikinga na madhara yanayoweza kupelekea athari katika mwili wako.

Msikilize hapo chini Dkt. Kiili akielezea madhara ya kutumia vipodozi vyenye madhara.

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea