Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

KMC yawajibu Stand United

Wednesday , 11th Jul , 2018

Klabu ya manispaa ya Kinondoni (KMC), imejibu tuhuma dhidi yao ya kumsajili mchezaji Ally Ally kutoka Stand United wakati akiwa na mkataba wa miaka miwili na klabu yake.

KMC kupitia kwa mkurugenzi wake, Walter Urio imesema kuwa wamemsajili Ally Ally baada ya kujiridhisha kuwa yuko huru, alipovunja mkataba na klabu yake na ushahidi wanao huku wakiitaka Stand United ilete ushahidi wao mezani watawajibu.

“Sisi tumemsajili Ally Ally baada ya kujiridhisha kuwa yuko huru, alivunja mkataba na Stand United baada ya kudai malimbikizo ya mshahara wake wa miezi minne na ushahidi wa nakala ya barua ya kuvunja mkataba ipo SPUTANZA na TFF kwahiyo wao kama bado wanadai ni mchezaji wao basi wapeleke ushahidi TFF “. Amesema Urio.

Stand United kupitia kwa mwenyekiti wa kamati ya usajili, Mbasha Matutu ulionesha kusikitishwa juu ya usajili huo kwani hawakuwa na taarifa yoyote juu ya kuondoka kwake Shinyanga kuja Dar es salaam na kusaini KMC.

Matutu pia amekana tuhuma za kushindwa kumlipa mshahara wa miezi minne mchezaji huyo kuwa ni sababu iliyopelekea kuvunja mkataba naye huku akisisitiza kuwa wao walikuwa wakimlipa mshahara wake kila mwezi kama kawaida na hawana deni lolote kwake.

Ally Ally amesaini mkataba wa mwaka mmoja kuitumikia klabu ya KMC ambayo imepanda kucheza ligi kuu Tanzania Bara kuanzia msimu ujao wa 2018/19.

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa