Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Portland na Team Kiza kuwapindua wababe wa 2017 ?

Sunday , 29th Jul , 2018

Timu nne zilizofuzu hatua ya nusu fainali ya Sprite Bball Kings leo Julai 29, 2018 zinashuka dimbani kucheza mechi za kwanza kati ya zile tatu za kuamua ni timu gani zinakwenda hatua ya fainali huku kukiwa na timu mbili zilizofika hatua hii kwa mara ya pili.

Team Kiza wenye jezi nyeupe walipocheza na DMI waliovaa nyeusi kwenye mechi ya robo fainali.

Katika mechi hizo zitakazopigwa kwenye uwanja wa taifa wa ndani, mechi ya kwanza itakuwa ni kati ya timu iliyocheza nusu fainali 2017, Flying Dribblers dhidi ya wageni wa hatua hii Team Kiza huku mechi ya pili ikiwa ni wageni wengine wa nusu fainali, timu ya Portland wakiwakaribisha mabingwa watetezi Mchenga Bball Stars.

Flying Dribblers wanacheza nusu fainali yao ya pili mfululizo wakiwa na kumbukumbu ya kutolewa na Mchenga Bball Stars mwaka 2017, ambao walikwenda kuwa mabingwa. Mwaka huu wamefanikiwa kufika hatua hii tena.

Portland wao waliishia hatua ya mchujo kwa mwaka 2017 lakini mwaka huu wamejipanga vyema wakiwa ndio timu iliyofunga pointi nyingi zaidi (257) tangu mashindano yaanze. Leo watakuwa na kibarua wakiikabili Mchenga Bball Stars ambao katika mechi mbili tu wamefunga pointi 201.

Kwa mujibu wa kamati ya maandalizi kutoka East Africa Televison kwa kushirikiana na shirikisho la Kikapu nchini (TBF), maandalizi yamekamilika na mechi zitaanza saa 10:00 jioni. Mechi za nusu fainali zinacheza kwa mtindo wa 'Best of three', lakini ikitokea timu moja ikashinda mechi 2 za kwanza itakuwa imefuzu hatua ya fainali bila kucheza mechi ya tatu.

Sprite Bball Kings inadhaminiwa na kinywaji baridi cha Sprite na mshindi ataondoka na kitita cha shilingi milioni 10, mshindi wa pili milioni 3 na mchezaji bora 'MVP' akiondoka na shilingi milioni 2.
 

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea