Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

TFF yafanya maamuzi juu ya Yanga SC

Thursday , 12th Jul , 2018

Kikao cha Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kimemuondoa Clement Sanga aliyekuwa mwenyekiti wa Bodi ya Ligi (TPLB) kwenye nafasi hiyo, kwa kukosa sifa baada ya klabu ya Yanga kuthibitisha Yusuph Manji kuwa mwenyekiti wa klabu hiyo.

Rais wa shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Wallace Karia

Hayo yameelezwa na Rais wa shirikisho hilo, Wallace Karia wakati alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam Julai 12, 2018 na kusema kwamba kutokana na hilo Sanga amepoteza sifa ya kuwa kiongozi wa bodi hiyo kwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi anapaswa awe Mwenyekiti wa klabu inayoshiriki ligi kuu.

"Tulipokea barua Julai 12 kutoka klabu ya Yanga ikidai kuwa Sanga hatambuliki kama Mwenyekiti wa klabu hiyo, wao Yanga wanamtambua Yussuf Manji ndiye Mwenyekiti wa klabu hiyo na katika nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi unatakiwa uwe Mwenyekiti wa klabu yako", amesema Karia

Vile vile, Rais wa shirikisho hilo Wallace Karia, ameielekeza kamati ya uchaguzi ya Yanga kuandaa uchaguzi wa kuziba nafasi hiyo.

Clement Sanga

Katika hatua nyingine, Karia amesema Kamati ya Utendaji imempitisha rasmi Wilfred Kidao kuwa Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) baada ya kukaimu kwa muda mrefu.

Maamuzi hayo ya Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) yamekuja  kufuatia mkutano uliofanywa Juni 10 wa wanachama wa Yanga na kusema bado wanamtambua Yussuf Manji kama Mwenyekiti wao.

HABARI ZAIDI

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu