Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Tumewasha moto wa tipa - Kocha Azam FC

Sunday , 15th Jan , 2017

Kocha Msaidizi wa Azam FC, Idd Nassor Cheche, aliyeiongoza timu hiyo kuchukua ubingwa wa Kombe la Mapinduzi, amesema moto waliouwasha kwenye kwenye michuano hiyo watauendeleza katika michuano ya ligi kuu Tanzania Bara na hakuna wa kuuzima.

Idd Nassoro Cheche

Cheche amesema moto huo waliouwasha ni wa tipa (ule wa kwenye viwanda vya mafuta) na hauwezi kuzimika huku akisema kuwa jambo kubwa lilipelekea mafanikio hayo kwa kikosi chake ni mshikamano, hali ya kujituma kwa wachezaji na kufuata maelekezo yake.

“Unajua unapokuwa binadamu na ukapata mafanikio makubwa kama haya ndani ya muda mfupi lazima uwe na furaha, nawashukuru wachezaji wangu kwa kazi kubwa waliyofanya na mshikamano na hali ya kujituma na jitihada walizozionesha, kwa hakika hivyo ndivyo vilivyotupa ubingwa,” alisema.

Kocha huyo aliyekuwa akisaidiana na Kocha wa Makipa Idd Abubakar, kufanya kazi hiyo kubwa hadi kufikia mafanikio hayo, kuanzia kwenye ligi watakuwa chini ya Kocha Mkuu mpya, Mromania Aristica Cioaba, aliyechukua mikoba ya Mhispania Zeben Hernandez, aliyesitishiwa mkataba pamoja na benchi lake zima la ufundi.

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea