Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Waliosoma shule binafsi wapatiwa mikopo

Thursday , 17th Oct , 2019

Jumla ya wanafunzi 1,890 waliosoma katika shule binafsi kwa ufadhili na wakathibitisha taarifa zao, Bodi ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu (HESBL), kama ilivyokuwa imeagizwa na Waziri wa Elimu, Joyce Ndalichako wamekwishapatiwa mikopo.

Taarifa hiyo imetolewa leo Oktoba 17, 2019, na Mkurugenzi Mtendaji wa bodi hiyo Abdul-Razaq Badru, ambapo amesema kuwa mpaka sasa wamekwishatoa mikopo yenye thamani ya Shilingi bilioni 113.5 kwa wanafunzi 30,675 wa awamu ya kwanza ya masomo kwa mwaka 2019/2020.

Katika makundi maalum pia tuna wanafunzi 1,890, sawa na asilimia 6 ya wanafunzi 30,675 wa awamu ya kwanza, ambao walisoma shule binafsi lakini kutokana na hali duni ya uchumi, walifadhiliwa na walithibitisha kwa kuweka nyaraka sahihi'' amesema Badru.

Aidha Badru amewataka waombaji wa mikopo, kufungua akaunti zao binafsi ili waweze kupata taarifa za mikopo kwa urahisi zaidi.

Pamoja na tovuti, wanafunzi wanaweza kufungua akaunti zao walizooombea mkopo mtandaoni maarufu kama SIPA na kuona walivyopangiwa na tunaanza kupeleka fedha vyuoni kesho kwa kuwa Serikali imeshatukabidhi Shilingi bilioni 125, ambazo tuliomba kwa malipo ya kati ya Oktoba hadi Disemba mwaka huu'' amesema Badru.

Kwa mwaka huu wa masomo, Serikali imetenga kiasi cha Shilingi bilioni 450, zinazolenga kuwanufaisha jumla ya wanafunzi 128,285, kati yao zaidi ya wanafunzi 45,000 ni wa mwaka wa kwanza na wengine 83,285 ni wanaoendelea na masomo

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea