Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Walioonesha ubovu wa barabara Ngorongoro kukamatwa

Sunday , 16th Feb , 2020

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo, ameliagiza Jeshi la Polisi mkoani humo kuhakikisha linawachukulia hatua stahiki wale wote walioshiriki katika zoezi la usambazaji wa video mitandaoni, zinazoonesha ubovu wa miundombinu katika Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo.

RC Gambo amesema kuwa haikuwa vibaya kukosoa ubovu wa miundombinu hiyo bali haikuwa jambo jema kusambazaa video hizo mitandaoni ili hali kuna viongozi ambao walipaswa kupelekewa taarifa hizo na suala hilo likapatiwa ufumbuzi.

"Changamoto hii ya barabara iko maeneo yote duniani sio Tanzania pekee, wapo baadhi ya watu kama Tour Guide ambao wamekuwa wakitoa taarifa bila kibali cha mamlaka husika, Mataifa mengine siyo kwamba hakuna mabaya, sema wanachagua ni kipi cha kupeleka Duniani, namuagiza RPC awachukulie hatua wale wote wanaochafua picha ya nchi, mimi nawachukulia kama wahujumu uchumi" amesema RC Gambo.

Hivi karibuni zilisambaa video mbalimbali katika mitandao ya kijamii, zikionesha ubovu wa miundombinu ya barabara katika hifadhi hiyo.

Tazama Video hii hapa chini
 

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea