Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mkude kutojiunga kambini Stars, kocha azungumza

Tuesday , 17th Mar , 2020

Kikosi cha timu ya taifa, Taifa Stars kinaendelea na mazoezi Jijini Dar es Salaam kujiandaa na mchezo wa kuwania kufuzu michuano ya AFCON dhidi ya Tunisia na michuano ya CHAN nchini Cameroon.

Jonas Mkude

Jumla ya wachezaji 35 waliitwa kujiunga na Taifa Stars katika mchezo huo na wachezaji wengi wamewasiri kambini isipokuwa wachezaji wa Yanga pamoja na kiungo wa klabu ya Simba, Jonas Mkude ambaye hakuna taarifa rasmi ya kwanini hajajiunga na kambi.

Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Etienne Ndayiragije amesema kuwa hana taarifa rasmi kwanini mchezaji huyo hajawasiri kambini na yeye anasubiri taarifa kujua alikuwa wapi.

"Wachezaji ambao hawajafika ni wengi sio Jonas Mkude peke yake, wapo wa Yanga pamoja na wengine wanafika leo jioni lakini Jonas tatizo ni kwamba wachezaji wenzake wamefika yeye hajafika", amesema Ndayiragije.

"Alisema anakwenda Morogoro lakini hatujawa na uhakika aliko pamoja na sababu za kwanini hajafika, lakini kuna msemaji na wale wanaohusika watawapa taarifa. Mimi siwezi kuliongelea jambo ambalo sijalijua vizuri", ameongeza.

Kwa mujibu wa taarifa ya Shirikisho la Soka Barani Afrika CAF, mchezo huo wa kuwania kufuzu AFCON kati ya Taifa Stars dhidi ya Tunisia umeahirishwa kutokana na tishio la virusi vya Corona huku pia michuano ya CHAN iliyotakiwa kufanyika nchini Cameroon kuanzia Aprili 4 -25, imeahirishwa.

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea