Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Yanga itakavyokamilisha ujenzi, viwanja na M/Makuu

Monday , 23rd Mar , 2020

Klabu ya soka ya Yanga ipo katika mpango mkubwa wa ujenzi wa kituo cha soka pamoja na ofisi za Makao Makuu ya klabu katika vipindi tofauti kuanzia hivi karibuni.

Eneo la viwanja vya Yanga vitakapokamilika

Kituo hicho kitakachojengwa katika eneo lao lililopo Kigamboni, Dar es Salaam, kitakuwa na jumla ya viwanja viwili vya mazoezi vya soka, hosteli za wachezaji pamoja na bwawa la kuogelea lenye viwango vya Olympic pamoja na viwanja vya Mpira wa Kikapu na Mpira wa Pete.

Akizungumzia kuhusu mipango hiyo, mmoja wa wajumbe wa Kamati ya Ujenzi na Miundombinu wa klabu hiyo, Said Mrisho amesema kuwa kila kitu kipo sawa na kinachosubiriwa ni mvua kupungua ili kuanza kwa awamu ya kwanza ya ujenzi ambayo itahusisha viwanja hivyo viwili.

"Tunataka kuanza kujenga viwanja viwili vitakavyokidhi vigezo vya FIFA na CAF na kuandaa mashindano ya Kimataifa ya U-17 na timu yetu ya wanawake, cha kwanza ni cha nyasi bandia na kingine ni cha nyasi asilia", amesema Mrisho.

"Utekelezaji haufanyiki kwa pamoja, utaenda kwa hatua ambapo kwa mwaka huu sisi kama kamati tumeshauri tuanze na viwanja vya mazoezi na suala la upatikanaji wa fedha ni la uongozi wa klabu. Mungu akipenda mvua zikiisha tutaanza ujenzi na mpaka kufikia Disemba mwaka huu utakuwa umekamilika", ameongeza.

Kuhusu suala la kurekebisha ofisi za Makao Makuu ya klabu hiyo, Said Mrisho amesema kamati yake imeshauri kuwa suala la ujenzi wa ofisi mpya katika eneo la Makao Makuu litafuata baada ya kukamilika kwa mradi wa serikali katika eneo la Jangwani na kwamba hivi sasa nguvu kubwa inaelekezwa Kigamboni.
 

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea