Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Simba yahusishwa na washambuliaji 2 Kimataifa

Wednesday , 20th May , 2020

Katika kipindi cha mwezi mmoja wa Mei, 2020 klabu ya Simba imehusishwa na kuwasajili washambuliaji wawili wa kimataifa ili kuimarisha kikosi chake kuelekea msimu ujao wa ligi pamoja na michuano ya Kimataifa.

Justin Shonga (kushoto) na Michael Sarpong (kulia)

Mwanzoni mwa mwezi Mei 2020, kulikuwepo na tetesi za Simba kuhusishwa na kumsajili mashambuliaji wa klabu ya Orlando Pirates, Mzambia Justin Shonga. Mchezaji huyo ana umri wa miaka 23 na ameichezea timu ya taifa ya Zambia takribani mechi 24 na kufunga mabao 13 tangu mwaka 2017.

Pia hivi karibuni klabu ya Simba imehusishwa na tetesi za kumsajili mshambuliaji wa klabu ya Rayon Sports raia wa Ghana, Michael Sarpong (24) ambaye ndiye alikuwa mfungaji bora wa msimu wa 2018/19 akiwa amefunga mabao 16. Pia mchezaji huyo amekuwa akihusishwa na kusajiliwa na mahasimu wao Yanga.

Imeelezwa kuwa Simba imethamiria kuwa na safu bora ya ushambuliaji hasa katika michuano ya Klabu Bingwa Afrika msimu ujao ili izidi katika hatua ya makundi ambayo iliishia msimu huu.

Baadhi ya wachezaji ambao wanatajwa huenda wakaachwa na Simba ili kupisha usajili huo ni pamoja na Haruna Shamte, Kennedy Juma, Tairone Santos, Shiza Kichuya, Yusuf Mlipili ambao wamekuwa hawana nafasi za kudumua katika kikosi cha kwanza.

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea