Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Vita ya Simba na Yanga kwa mchezaji, wakala aeleza

Wednesday , 27th May , 2020

Klabu za Simba na Yanga ziko katika vita ya kuwania saini ya mlinzi matata wa klabu ya Coastal Union, Bakari Nondo Mwamnyeto kuelekea msimu ujao wa 2020/21.

Haruna Niyonzima wa Yanga, Luis Miquissone na Meddie Kagere wa Simba

Beki huyo amekuwa katika midomo ya wadau wengi wa soka msimu huu kutokana na umahiri wake wa kuzuia na kuisaidia klabu ya Coastal Union kufikia katika nafasi nzuri msimu huu.

Wakala wa mchezaji huyo ambaye pia ni mchezaji wa zamani wa soka katika mkoa wa Tanga, Kasa Mussa amethibitisha mchezaji huyo kuhitajika na klabu hizo kubwa nchini na kwamba kinachosubiriwa ni msimu kumalizika ili waweze kukamilisha dili na moja ya klabu hizo.

Amesema kuwa Yanga wameonesha nia ya kumuhitaji pamoja na Simba lakini mpaka sasa hajafikia makubaliano ya dau la uhamisho na klabu ya Yanga ambao ndio wako katika mazungumzo mazuri.

Klabu ya Yanga imesharejea mazoezini jana baada ya kukamilisha vipimo vya wachezaji na benchi la ufundi, hivyo leo mazoezi rasmi yanatarajia kuanza sambamba na Simba na Azam FC ambao wanatarajia pia kuanza mazoezi yao leo.

Pia Serikali kupitia Baraza la Michezo Tanzania BMT inatarajia kutoa mwongozo rasmi kuelekea kurejea kwa Ligi Kuu Tanzania Bara na Ligi Daraja la Kwanza na la Pili, ikiwemo suala la mwongozo wa afya.
 

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea