Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Solskjaer amehoji maamuzi ya vilabu vya EPL

Friday , 30th Oct , 2020

Kocha wa Manchester United Ole Gunnar Solskjaer amehoji ni kwanini vilabu vya Ligi Kuu England vilipiga kura ya kupinga kufanya mabadiliko ya wachezaji wa 5 kwenye michezo ya EPL msimu huu.

Mchezo dhidi ya Arsenal siku ya Jumapili utakuwa wa 100 kwa kocha Ole Gunnar Solskjaer akiisimamia Man United kama kocha mkuu

Kura ya vilabu kupinga kanuni ya kufanya mabadiliko ya wachezaji wa 5 kwa mchezo mmoja ilipigwa mwezi Agosti na vilabu vinavyoshiriki ligi kuu England EPL na kutumia kanuni ya zamani ya kufanya mabadiliko ya wachezaji wa 3.

Lakini kanuni hiyo bado inatumika kwenye michuano ya klabu bingwa ulaya na ile ya Europa league.

“Sielewi na siamini kwanini ilipigwa kura ya kupinga, tunapaswa kuwalinda na kuwafikiria wachezaji ” alisema Solskjaer alipokuwa akiongeza na waandishi wa habari kuelekea mchezo dhidi ya Arsenal.

Kutokana na mlipuko wa Covid-19 ambao ulisababisha ligi mbali mbali kusimama Duniani kote na wachezaji kushinda kufanya mazoezi, ili kulinda afya za wachezaji kuwaepusha na majeruhi, vilabu vilipewa nafasi ya kufanya mabadiliko ya wachezaji wa 5 kwa mchezo kutoka wa 3.

Shirikisho la soka Dunia FIFA lilitoa ruhusa kwa ligi mbali mbali kendelea kutumia kunani hiyo kwa muda mpaka mwishoni mwa msimu huu wa 2020-21, lakini vilabu vya England vilipiga kura ya kupinga kununi hiyo na kutumia kanuni ya zamani ya mabadiliko ya wachezaji wa 3.

Ole Gunnar sio kocha wa kwanza kuhoji juu ya umuhimu wa mabadiliko ya wachezaji wa 5 kwani hata Kocha wa Manchester City Pep Guardila anaamini afya za wachezaji zinapaswa kulindwa huku Kocha wa Chelsea, Frank Lampard akisisitiza makosa yalifanyika kupinga kanuni ya mabadiliko .

HABARI ZAIDI

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu