Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Hospitali na Daktari waingia kwenye mikono ya JPM

Saturday , 30th Jan , 2021

Rais Dkt. John Magufuli amemuagiza Waziri wa Afya Dkt Dorothy Gwajima, kuhakikisha anawafuatilia madaktari walioacha kazi katika hospitali ya rufaa mkoa wa Tabora kwa sababu ya maslahi na kuhamia hospitali binafsi na ikiwezekana afungiwe yeye pamoja hospitali aliyoikimbilia.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli

Kauli hiyo ameitoa hii leo Januari 30, 2021, wakati akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo la magonjwa ya dharura katika hospitali hiyo na kwamba haiwezekani serikali ipoteze pesa kwa ajili ya kusomesha madakatari na wao badala ya kuwatumikia wananchi wanaanza kuwa wabinafsi kwa kutaka maslahi makubwa.

"Mfuatilie huyo daktari aliyekimbia hapa, uifuatilie na hiyo hospitali ikiwezekana tunamfungia huyo daktari na tunaifungia na hiyo hospitali aliyoenda kutibia ili watu waanze kujifunza kwamba wizara ya afya siyo ya kuchezea tu, unamsomesha mtu kwa fedha za watanzania halafu anasema maslahi madogo", amesema Rais Magufuli.

Aidha Rais Dkt. Magufuli, "Madaktari wote wanapata mkopo kwa asilimia 100, unasoma pale kwa miaka mitano ukishatoka pale unasema maslahi madogo, si ungekimbia wakati unasoma hela yetu umekula halafu unasema maslahi madogo, nia ya serikali ni kuboresha maslahi lakini unaanza na kimoja, unaboresha maslahi wakati huna majengo wala vifaa vya kutosha".

HABARI ZAIDI

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu