
Mkuu wa mkoa wa Mtwara Gelasius Byakanwa
Kauli hiyo wameitoa mbele ya Mkuu wa mkoa huo Gelasius Byakanwa, wakati akizungumza na waganga hao na kuwasihi Watanzania kuacha tabia ya kutegemea mataifa ya nje katika masuala ya utafiti na badala yake wawatumie waganga wa tiba asili hasa katika kipindi hiki cha magonjwa ya mlipuko kwani waganga hao wanazo dawa za kutibu magonjwa ya mfumo wa hewa na upumuaji.
Wiki moja tangu mkuu wa mkoa huo kutoa tangazo la kuonana na waganga wa tiba asili, jumla ya waganga 41 kutoka maeneo mbalimbali wamejitokeza kwa ajili ya utambuzi wa dawa zao.