Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Manchester United yafanya usajili wa kwanza

Tuesday , 5th Jul , 2022

Klabu ya Manchester United imekamilisha na kutangaza usajili wa beki wa kushoto Tyrell Malacia kutoka klabu ya Feyenoord ya Uholanzi kwa ada ya uhamisho iya pauni milioni 12 zaidi ya Bilioni 33 kwa pesa za kitanzania amesaini mkataba wa miaka 4.

Tyrell Malacia amejiunga na Manchester United kwa mkataba wa miaka 4

Taarifa ya Manchester united juu ya usajili wa beki huyu raia wa Uholanzi mwenye umri wa miaka 22 imesema.

''Manchester United tunapenda kuthibitisha kwamba Tyrell Malacia amejiunga na klabu yetu, na amesaini mkataba hadi Juni 2026 na chaguo la kuongeza mwaka mmoja zaidi.’’ Imesema taarifa ya Manchester United

Malacia anakuwa mchezaji wa kwanza kusajiliwa Manchester United chini ya kocha mpya wa klabu hiyo Erik Ten Hag na anatarajiwa kuwa sehemu ya kikosi kitakacho safari siku ya Ijumaa kuelekea nchini Thailand na Australia ambako klabu hiyo itaweka kambi ya maandalizi ya msimu mpya (Pre-season).

Kwa upande mwingine mchezaji mwenye amefurahishwa kujiunga na Manchester United.

''Ni hisia ya tofauti sana kujiunga na Manchester United. Huu ni ikurasa mpya kwangu, Ligi mpya na wachezaji wenza wapya na kocha mzuri anayetuongoza. Namjua kutokana na kucheza dhidi ya timu yake kwenye Eredivisie (Ligi kuu Uholanzi), sifa alizonazo na kile anachokitaka kutoka kwa wachezaji wake.’’Amesema Malacia

Malacia ameichezea Feyenoord jumla ya michezo 136 katika misimu 5 na amefunnga mabao 4, lakini pia ameichezea timu ya taifa ya Uholanzi jumla ya michezo 5 kati ya mwaka 2021 mpaka 2022.

HABARI ZAIDI

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu