Monday , 5th Sep , 2022

Serikali imeagiza kuanzia leo September 5, 2022 mifugo yote inayochinjwa katika machinjio ya Vingunguti nyama yake yote itatakiwa kuuzwa katika eneo maalum lililojengwa pembezoni mwa machinjio hiyo.

Mkuu wa Wilaya ya Ilala Ng'wilabuzu Ludigija

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Ng'wilabuzu Ludigija leo, huku akieleza kuwa kwa sasa serikali imetoa mwezi mmoja kwa wafanyabiashara hao kutolipa gharama zozote katika maeneo hayo mapya ya kuuzia nyama lengo ikiwa kuweka utulivu kwa wafanyabiashara.
Hata hivyo eneo la kuuzia nyama hiyo limeonekana dogo hivyo kuagiza Tena Halmashauri ya Jiji la Ilala kuchukua eneo jingine na kuwafidia wanachi haraka iwezekanavyo.