Wednesday , 18th Jan , 2023

Makamu wa rais wa Gambia Badara Alieu Joof amefariki dunia nchini India alikokua akipatiwa matibabu, rais Adama Barrow ametangaza.

Hayati Badara Alieu Joof

Makamu huyo wa rais alifariki baada ya kuugua kwa muda mfupi, ingawa Bw Barrow hakutaja ikiwa alikuwa akipokea matibabu nchini India.

Bw Joof hakuonekana hadharani kwa miezi kadhaa,  ikiwa ni baada ya kuchaguliwa na Rais  Barrow  kama makamu wa rais baada ya kuchaguliwa tena mnamo Desemba 2021 kwa muhula wa pili.

Mwezi Juni, Bw Joof alielezea kutoridhishwa na mwenendo wa masuala ya umma, akisema Raia wa Gambia walikuwa na matarajio makubwa na  mwendelezo wa mambo yale yale kiutendaji  haitasababisha mabadiliko makubwa.