Wednesday , 18th Jan , 2023

Mmoja wa watoto wa rais wa Guinea ya Ikweta amekamatwa kwa tuhuma za kuuza ndege kinyume cha sheria mali ya shirika la ndege la taifa.

Rais Teodoro Obiang Nguema alitwaa madaraka 1979

Vyombo vya habari vya serikali vimesema Ruslan Obiang Nsue anadaiwa kuuza turboprop yenye siti 74 kwa kampuni iliyoko katika visiwa vya Canary.

Uchunguzi ulianzishwa mwaka jana ilipogundulika kuwa ndege hiyo ilikuwa imepotea wakati ikifanyiwa matengenezo ya kawaida nchini Uhispania.RPU

Mshukiwa huyo alikuwa akiendesha shirika la ndege la taifa nchini Equatorial Guinea, nchi ambayo iko imara mikononi mwa familia ya Rais Obiang Nguema ambaye amekuwa madarakani kwa miaka 43.