Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Watoto kupata taarifa za matukio ya ukatili

Saturday , 28th Jan , 2023

Jeshi la Polisi mkoani Arusha limeungana na watoto wanaoishi katika kituo cha kulelea yatima kijulikanacho kwa jina la Maasai Girls Rescue Center kilichopo wilaya ya Karatu kwa lengo la kuwaleta karibu watoto na jeshi hilo ili kupata taarifa za matukio ya ukatili wa kijinsia.

Baadhi ya Askari wa Jeshi la Polisi Arusha wakiwa na watoto yatima

Tukio hilo limefanyika leo Januari 28, 2023, Mkuu wa polisi wilaya ya Karatu Mrakibu Mwandamizi wa Polisi SSP Radegunda Marandu, amesema jeshi hilo limetoa misaada mbalimbali kwa yatima hao ikiwa ni mkakati wa kuifanya jamii kuwa karibu nao.

SSP Marandu amebainisha kuwa pamoja na kuwa jeshi hilo linahusika na ulinzi wa raia na mali zao pia wanalo jukumu la kushirikiana na wananchi katika matukio  ya kijamii ikiwemo la kuonyesha upendo kwa yatima ambapo watakua huru kueleza changamoto mbalimbali zinazowakabili ikiwemo za ukatili.

Sambamba na hilo pia ametoa onyo kwa watu wachache ambao wana tabia ya kuwafanyia watoto vitendo vya ukatili kuacha mara moja kwani jeshi hilo lipo makini na litachukua hatua kali za kisheria dhidi yao.

Naye Bwana Elisante Loi, meneja wa kituo hicho amesema msadaa uliotolewa utawafanya watoto hao kujua kuwa polisi ni sehemu ya jamii hivyo watakua huru kueleza changamoto mbalimbali zinazowakabili kwa jeshi hilo bila kuogopa.
 

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea