Chama: 
TADEA
Mgombea Mwenza (Makamu wa Rais): 
Ali Makame Issa
Idadi Ya kura: 
0

Georges Gabriel Bussungu ni mwanasiasa  anayeamini katika mabadiliko ya fikra

Amezaliwa Aprili 23,1957 Kituo cha afya Makongoro Nyamagana Mwanza

Mama yake anaitwa Modesta Manungwa Nabeji na Baba yake ni Gabriel Fella Bussungu

Februari 05,1967 akiwa na miaka 9 alishiriki matembezi kuunga mkono azimio la Arusha

1969 alijiunga na vijana TANU na kuchaguliwa kuwa mwenyekiti wa vijana wa tawi

1970 akawa mwenyekiti wa TANU wilaya ya Nzega

Alikuwa na ndoto ya kuwa Kasisi wa Kanisa Katoliki

Amewahi kufanya kazi wizara ya viwanda na biashara akiwa Afisa biashara

Alijiunga na JKT na pia alishiriki vita vya Kagera

Ana stashahada ya uongozi,utawala, uhasibu alizozipata mwaka 1979,1986,

Pia ana shahada ya uongozi wa biashara aliyoipata mwaka 1990 chuo kikuu Mzumbe

Amewahi kuwa Katibu Tawala wa Mikoa ya Singida, Manyara kabla ya kustaafu kisheria mwaka 2017

Amekuwa mwanachama wa CCM tangu akiwa mtoto hadi mwaka 2021 alipojiunga rasmi ADA TADEA

Mwaka 2022 alichaguliwa na chama chake kuwa Naibu Katibu Mkuu

Mume wa Yasinta Medard Chuleha na Baba wa watoto kumi