
Katibu Mkuu Wizara wa Afya Prof. Abeli Makubi
Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dodoma, Katibu Mkuu Wizara wa Afya Prof. Abeli Makubi, amesema kuwa katika Kampeni hiyo wizara itashirikiana na Wizara ya TAMISEMI lengo likiwa ni kuwafikia wananchi kwenye mitaa yao, vitongoji pamoja vijiji vyao
Prof. Makubi amesema kampeni hiyo itawashirikisha wasanii mbalimbali,viongozi wa Kijiji na vikundi mbalimbali vya kimila ili kuwezesha kuwafikia wananchi kwa urahisi
Aidha Prof. Makubi amesema kuwa mpaka sasa watu waliopatiwa chanjo ya UVIKO-19 ni asilimia 2.2 huku malengo ni kufikia asilimia 60.