Ijumaa , 14th Oct , 2022

October 14 ya mwaka Taifa la Tanzania huadhimisha kumbukumbu ya kifo Cha baba wa Taifa hayati Mwl Kambarage Julius Nyerere ambapo hii Leo Wakazi wa Dar es salaam wamemtaja kama mhifadhi namba Moja.

Hayati baba wa Taifa Mwl Julius Kambarage Nyerere

Nyumbani Kwa mwalimu Nyerere Magomeni Dar es Salaam Nyumba ya kwanza iliyotajwa kufanyia harakati mbalimbali za uhuru na hapa baadhi ya Wakazi wa Dar es Salaam wanamzungumza mwalimu  kama mhifadhi   namba Moja katika maliasili za nchi ikiwemo hifadhi,madini pamoja na Mali kale.

Pamoja na hivyo bado serikali imekuwa ikifanya mikakati mbalimbali ili kuhakikisha vijana wa leo wanafahamu nini ilikuwa chimbuko la Mwalimu Nyerere Kupenda kukutana katika michezo mbalimbali ili kuimarisha hali ya kisiasa kipindi kile cha ukoloni.

Hata hivyo wazee hao wamewataka vijana wa sasa waliopata nafasi ya masomo kuzitunza falsafa na maadili aliyokuwa nayo Mwalimu Nyerere Enzi za utawala wake.