
Mmoja wa wananchi amesema licha ya kuwepo mradi unaojengwa kijijini hapo, mradi umechukua mda mrefu na kusababisha wananchi kuendelee kukosa maji na kutumia ya visima na mito yasiyo salama.
Akitolea ufafanuzi wa mradi unaotekelezwa kutokamilika kwa wakati, Meneja wa wakala wa maji na usafi wa mazingira vijijini RUWASA mhandisi Mathiaus Mwenda amesema mradi umefikia asilimia 90
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Uvinza Hanafi Msabaha amekiri kata hiyo kutokuwa na huduma ya maji, na kwamba mradi unaotekelezwa licha ya kutumia gharama kubwa bado umekuwa na kusua sua kukamilika
Waziri wa maji Jumaa Aweso ametoa maelekezo kwa RUWASA na kutaka ndani ya wiki moja vifaa viwe vimefika na mradi uanze kazi mara moja ya kuhudumia wananchi.