
Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Yanga, Jerry Muro amesema, waamuzi watakaosimamia mchezo huo watatokea visiwa vya Shelisheli huku kamishna wa mchezo akitokea nchini Afrika kusini.
Muro amesema, katika mchezo huo wao kama timu wenyeji kwa kushirikiana na Shirikisho la Soka nchini TFF wameamua kuweka viingilio ambavyo vitakuwa rafiki kwa mashabiki na kuwafanya mashabiki kufika kwa wingi Uwanjani kwa ajili ya kuipa Sapoti Klabu ya Yanga