Ijumaa , 20th Jan , 2023

Raia wa Zambia sasa watashuhudia kukatika kwa umeme kwa saa nane badala ya saa 12 kwa siku, waziri wa nishati ametangaza, akihusisha mabadiliko hayo na kuongeza uwezo.

"Pamoja na kurejeshwa kwa jenereta ya megawati 150 katika kampuni ya Maamba Collieries Limited, uzalishaji  kwa sasa  ni megawati 1,910 kinyume na mahitaji ya umeme ya megawati 2,380," alisema Waziri wa Nishati, Douglas Syakalima.

Hii inamaanisha kuwa watu wanaweza kutarajia kukatika kwa umeme mara mbili kwa siku kila moja inayodumu kwa saa nne. Bw Syakalima pia amesema kuwa  viwango vya maji katika Bwawa la Kariba vinaongezeka kutokana na mvua kubwa.

Wiki mbili zilizopita kampuni ya huduma za umeme ya Zambia, Zesco Limited, ilitangaza saa 12 za mgawo wa umeme kutokana na kazi za matengenezo katika maporomoko ya Maamba Collieries pamoja na viwango vya chini vya maji katika Bwawa la Kariba, linalozalisha umeme wa maji katika kaunti hiyo.