Wadaiwa sugu elfu 26, wadakwa
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo nchini (HESLB), Abdul Razaq Badru amesema kuwa, kuanzia mwaka jana mpaka sasa wamefanikiwa kuwapata wadaiwa sugu 26,000 wa mikopo ya elimu ya Juu na bado wanaendelea na msako wa kuwatafuta.