Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kanisa katoliki latoa tamko kuhusu ushoga

Monday , 3rd Dec , 2018

Kiongozi wa kanisa katoli duniani, Papa Francis, ametoa tamko kuhusu viongozi wa kanisa hilo kujihusisha na ushoga, na kusema kwamba kanisa haliruhusu vitendo hivyo.

Akihojiwa na Mmishenari mmoja kutoka nchini Uhispania aliyejulikana kwa jina la Fernando Prado kuhusu wito wa kidini na vitendo vya ushoga kwa ajili ya kitabu anachoandika kinachoitwa 'Nguvu ya Utumishi' , Papa Francis amesema kwamba kanisa katoloki halitaruhusu mtu yeyote anayejihusisha na vitendo hivyo, kuingia kwenye utawa.

Papa amesema mahusiano ya jinsia moja ni jambo la "fasheni" ambalo sasa limeshika hatamu duniani, na kutaka makasisi kutii viapo vyao vya utawa (kutojihusisha na mapenzi).

“Hili suala la mahusiano ya kimapenzi ya jinsia moja ni kubwa sana, kwa sababu hiyo, Kanisa linawataka watu wenye tabia hizo (wapenzi wa jinsia moja) wasikubaliwe katika maisha ya ukasisi”, amesema Papa Francis.

"Katika jamii zetu, sasa inaonekana kuwa suala hili la mapenzi ya jinsia moja limekuwa fasheni. Mawazo kama hayo sasa yanaanza kupata ushawishi ndani ya kanisa, suala hili katu halina nafasi katika maisha ya watawa wetu." aliongeza Papa Francis.

Pamoja na hayo Papa Francis amesema kwamba iwapo mtu amnayejihusisha na mapenzi ya jinsia moja kutaka kuwa karibu na Mungu, yeye hawezi kumuhukumu.

"Kama mtu ni shoga na anataka ukaribu na Mungu na ana nia njema, mimi ni nani wa kuhukumu?," amesema Papa Francis.

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani