Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Wameambukizwa Ukimwi, nitawasemea" - Matiko

Friday , 15th Mar , 2019

Mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko amelituhumu jeshi la polisi kwa kuwafanyia unyanyasaji wa kingono, mabinti na wanawake wanaopelekwa katika vituo vya polisi pindi wanapokamatwa.

Mbunge Esther Matiko

Akizungumza na wanahabari, leo Machi 15, Matiko amesema kwamba, alipokuwa Segerea amekutana na malalamiko ya wanawake ya kwamba wamebakwa na kulawitiwa walipokamatwa na hata kuambukizwa maradhi.

Amesema kwamba vitendo vya unyanyasaji kwa mkoa wa Dar es salaam vimekithiri katika vituo vya Sitaki Shari, Kawe na kile cha Mabatini.

Ameongeza kwamba, "licha ya kulisema suala hili leo mbele ya wanahabari, kama muwakilishi wa wanananchi Bungeni atalifikisha jambo hilo ndani ya bunge ili waathiriwa wa vitendo hivyo wapatiwe haki yao

"Kuna kesi  nyingi sana, mabinti wanabakwa kwenye vituo vya polisi, kulawitiwa na hata kuambukizwa virusi vya ukimwi, nimesema nitalisema hili  bungeni na popote pale mpaka haki za mabinti hawa zitakapopatikana" Amesema Matiko.

Pamoja na hayo Matiko amelalamikia suala la watu wenye magonjwa wa akili kuchanganywa na wemye utimamu katika magereza hasa Segerea na kusema kunaweza kupelekea matatizo kwa mahabusu au wafungwa wengine ndani ya gereza.

Ameongeza kwamba Licha ya matatizo yanayoweza kusababishwa na wagonjwa hao, Serikali inapaswa kutumia sheria ya 'Insanity ACT 31' ambayo inatamka wazi kwamba mtu anayekamatwa akawa na matatizo ya akili apelekwe sehemu stahiki na siyo magereza.

Aidha Matiko amesikitika kuwepo na mahabusu wengi magerezani huku serikali ikitumia gharama kubwa kwa mahabusu ambao hawazalishi huku akisisitiza kwamba wanawake waliopo katika magereza hayo wengine ni wazazi ambao kwa kuwekwa muda mrefu bila kujua hatima ya kesi zao kunapelekea watoto wa mitaani.

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea