Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Hata Mungu anaipenda siasa - Dkt. Mashinji

Saturday , 5th Nov , 2016

Katibu Mkuu wa CHADEMA Dkt. Vincent Mashinji, ameonesha kupingana na baadhi ya watu wanaodai kuwa siasa ni mchezo mchafu, kwa kusema kuwa dhana hiyo siyo sahihi kwa kuwa hata Mwenyezi Mungu aliyeumba kila kitu, anaipenda na ndiyo maana akairuhusu.

Dkt. Vincent Mashinji - Katibu Mkuu CHADEMA

 

Dkt. Mashinji alitoa kauli hiyo hivi karibuni kupitia kipindi cha KIKAANGONI kinachurushwa kupitia ukurasa wa Facebook wa EATV, ambapo mwananchi mmoja alitaka kujua mtazamo wake kuhusu dhana ya siasa kuwa mchezo mchafu na ni kwanini yeye aliamua kuingia kwenye siasa wakati akijua kuwa ni mchezo mchafu.

"Siasa siyo mchezo mchafu, hata kwa Mungu kuna siasa na ndiyo maana kulikuwa na utawala, hata yeye anapenda siasa ndiyo maana ameileta, siasa ni mfumo wa maisha, na ndiyo maana hakuna jambo lolote la maendeleo litaweza kufanyika bila siasa, siasa ni mfumo wa uongozi, siyo kweli kuwa siasa ni mchezo mchafu" Alijibu Dkt. Mashinji.

Aidha Mashinji ambaye ni daktari wa binadamu, amesema aliingia kwenye siasa miaka mingi iliyopita, na kwamba siyo mgeni kama ambavyo watu wengi wanadhania na kuongeza kuwa awali alikuwa ni mwanachama wa CCM lakini alipoona anaweza kuwa kiongozi na kusaidia maendeleo alijiunga na CHADEMA kwa kuamini kuwa ni chama kinachoweza kuliletea taifa maendeleo.

"Nimewahi kuwa mwanachama wa CCM, lakini ni katika kipindi ambacho ilikuwa ni lazima uwe na kadi ya CCM ili upate huduma au fursa fulani, kwahiyo nilikuwa na kadi lakini sikuwa na mapenzi na CCM" Alisema Dkt Mashinji na kuweka wazi kuwa yeye bado ni mwanataaluma katika fani ya udaktari na pia ni mtendaji wa chama ambaye hahitaji kuwa mtu wa majukwaani bali mtu anayefanya kazi kimyakimya.

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani