Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wachezaji wa Man United watawala benchi la ufundi

Monday , 11th Feb , 2019

Manchester United ni moja ya vilabu ambavyo wachezaji wake wengi wa zamani wameingia kwenye fani ya ukocha huku wengi wao wakifanya vizuri na wengine kufanya vibaya kiasi cha kufukuzwa.

Moja ya majukwaa maarufu ya uwanja wa Old Trafford maarufu kama ngome ya Ferguson.

Moja ya wachezaji wa zamani wa Manchester hususani wale waliocheza kwenye 'Class of 1999' ni Gary Neville ambaye alifikia ngazi ya kuifundisha timu ya Valencia ya Hispania, lakini hakudumu sana alifukuzwa kazi kutokana na matokeo mabovu.

Mchezaji mwingine ni Ryan Giggs ambaye alianza maisha ya ukocha ndani ya Man United, akifanya kazi na Louis van Gaal lakini baada ya kutimuliwa kwa kocha huyo Giggs pia aliondoka haswa baada ya ujio wa Jose Mourinho. Kwasasa Giggs ni kocha wa timu ya taifa ya Wales.

Wakati hao wakienda kuwa makocha nyota mwingine wa Man United ambaye yupo kwenye uongozi wa soka ni Edwin van der Sar  ambaye ni Mtendaji mkuu wa klabu ya soka ya Ajax ya Uholanzi.

Mbali na hao, leo Februari 11, 2019 kiungo wa zamani wa timu hiyo Paul Scholes, ametangazwa kuwa kocha wa timu ya Oldham Athletic Club ya England kwa mkataba wa mwaka mmoja na nusu. Oldham inashiriki 'League Two' ya nchini humo.

Anayekamilisha orodha hiyo ya nguli wa Manchester United wanaotamba kwenye vilabu ni Ole Gunnar Solskjær ambaye anaifundisha Man United kama kocha wa muda na ameisaidia kutoka nafasi ya 8 hadi ya 4 ndani ya mechi 10.

Kwasasa Ole Gunnar anasaidiwa na nyota wengine wa timu hiyo ambao ni Mike Phelan aliyecheza miaka 1989–1994 pamoja na Michael Carrick.

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani