Wachezaji wa Yanga na Zesco kwenye mechi ya leo
Zahera amesema hayo leo Septemba 14, 2019 baada ya mchezo wa kwanza wa hatua za awali kuwania kufuzu hatua ya Makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Zesco ambao umeisha kwa sare ya goli 1-1.
''Hakuna kilichobadilika hata kama wamefunga na sisi tunapaswa kwenda kufunga kule Zambia na hata kama wasingefunga bado tulipaswa kwenda kufunga goli kwahiyo tutahakikisha tunafunga kwao'', - Zahera.
Mchezo wa marudiano utapigwa Septemba 27 huko Lusaka Zambia, ambapo mshindi wa jumla atasonga mbele katika hatua ya makundi.