Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Watu wenye ulemavu, S/Mtaa watupiana mpira

Thursday , 26th Sep , 2019

Watu wenye ulemavu wanaoishi maeneo ya Mzimuni, Kawe Jijini Dar es Salaam wameilalamikia serikali ya mtaa huo kuwaandikisha majina kwa ajili ya kupata msaada wa vitendea kazi na usafiri wa bajaji ili kujikwamua kibiashara lakini wanaishia kudanganywa.

Pili Adam

Wakizungumza na EATV & EA Radio Digital, wananchi hao wamesema kuwa Serikali ya mtaa imekuwa ikiwafuata na kuwaandikisha majina ili wapewe bajaji lakini mwisho wa siku wamekuwa wakiachwa kwenye vikao vya mwisho vya maamuzi ilhali wao ni wahusika wakuu.

"Serikali yetu ya mtaa inaishia kutuandikisha tu majina na kutuambia mtaletewa msaada lakini vikitokea vikao vya walemavu wanaenda wao wazima, walemavu wa Kawe wote masikini hakuna mwenye nafuu hata mmoja",  amesema Pili Adam ambaye ni moja ya watu wenye ulemavu wanaoishi mtaa huo.

Aidha, Pilli Adam ameongeza kuwa msaada mkubwa ambao utawasaidia wao ni kupatiwa bajaji, zitakazowawezesha katika usafiri na hata kujipatia kipato tofauti na kupewa pesa mkononi.

Hata hivyo EATV&EA Radio Digital imemtafuta Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mzimuni, Hassan Ngonyani ambaye amekanusha taarifa hizo na kusema.

"Mimi hiki kitu sikijui kabisa, mimi nilishawagawiaga maeneo kwa ajili ya uzalishaji mali ili waweze kujipatia rizki lakini wameuza yale maeneo", ameeleza Mwenyekiti wa mtaa huo. 

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani