Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mkuu wa Shule atafuna ada, Serikali yamjia juu

Tuesday , 19th Jan , 2021

Serikali mkoani Geita imeuagiza uongozi wa shule ya sekondari ya Geita Islamic, ifikapo kesho asubuhi iwasilishe stakabadhi za malipo ya mitihani ya wanafunzi, baada ya Mwalimu Mkuu wa shule hiyo kukiri kula ada za mitihani ya Taifa ya wanafunzi wa kidato cha Pili na cha Nne.

Afisa Elimu wa mkoa wa Geita, Arnold Msuya

Akizungumza hii leo Januari 19, 2021, Afisa Elimu wa mkoa wa Geita, Arnold Msuya, amesema kuwa kitendo cha mwalimu huyo kula ada hizo, kimepelekea wanafunzi hao kukosa matokeo yao yaliyotangazwa hivi karibuni na Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA), ambapo kutokana na hali hiyo akaelekeza suala hilo lishughulikiwe na wanafunzi wapate matokeo yao.

"Tulipokea malalamiko kutoka kwa wazazi wa wanafunzi hao kwamba walilipa ada ya mitihani lakini matokeo ya watoto wao hayakutoka, nimemuelekeza mmiliki wa shule hiyo ifikapo kesho saa 4:00 asubuhi alete risiti za malipo ili matokeo yao yatoke, kama mkuu wa shule alipokea ada na akatoweka nazo hilo si jukumu la mzazi tena ni jukumu la mwenye shule aliyeruhusu fedha zikusanywe na kuwekwa mfukoni", amesema Arnold.

Kwa upande wake, Meneja wa shule hiyo Mussa Mnyita, amesema kuwa wazazi walikamilisha malipo hayo kutokana na changamoto ya mwalimu huyo kutolipa malipo hayo NECTA na kwamba uongozi wa shule utawajibika kulipa malipo hayo.

 

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani